KUFIKIA MALENGO



SOMO: MAMBO YATAKAYOKUSAIDIA UFIKE UNAKOTAKA KUFIKA KWENYE MAISHA YAKO YA KIROHO NA KIMWILI AU UYAFIKIE MAFANIKIO YAKO ULIYOYAWEKA KWENYE MAISHA

Lengo la somo
Ni kukuonesha kuwa katika safari yoyote ile unayoianzisha kwenye maisha yako ili ufike salama unakotaka kufika unahitaji maandalizi mazuri au yakutosha, mikakati yenye nguvu na ramani itakayokuelekeza kufika unakotaka kufika, lakini pia unahitaji imani yaani uamini kwamba utafika unakotaka kufika.

Utangulizi
Watu wengi Sana kwenye dunia hii, huwa Na malengo kwenye maisha Yao yawezekana malengo ya biashara, kwenye huduma, familia au jambo lolote lile. Haitoshi tu kuwa na malengo ila hutamani kuyafikia hayo malengo au kufikia kiwango wanachotaka kufika. Wengi huweza kukwama kufika wanakotaka kufika kwa sababu ya kusikiliza sana sauti za duniani ambazo huwafanya kujijengea mitazamo hasi au wengine hukwama kwa sababu ya mikakati mibovu na isiyo na nguvu ya kuwafikisha wanakotaka kufika.

Mambo yatakayokusaidia kufika unakotaka kufika au kuyafikia malengo unayotaka kuyafikia kwenye maisha  yako ya kimwili na kiroho.


  • Ili ufike unakotaka kufika unahitaji nguvu za Mungu zitokanazo na chakula cha rohoni (Neno la Mungu) na uhakika wa kutosha ndani yako wa kufika unakotaka kufika kwa msaada wa Roho Mtakatifu.

1 Wafalme 19:4
“Lakini yeye mwenyewe akaendelea katika jangwa mwendo wa siku moja , akaenda akaketi chini ya mretemu .Akajiombea roho yake afe ,akasema ,Yatosha ,sasa, Ee BWANA ,uniondoe roho yangu ; kwa kuwa mimi si mwema kuliko baba zangu .Naye kajinyosha akalala chini ya mretemu; na tazama malaika akamgusa ,akamwambia ,inuka ule”

1 Wafalme 19:7
“Malaika wa Bwana akamwendea mara ya pili, akamgusa akasema, inuka, ule, maana safari hii ni kubwa mno
Baada ya Eliya kuwaua wale manabii wa Baali na kupata vitisho vya kuuliwa Eliya aliingiwa na hofu sana. Eliya alikimbia ili aiokoe roho yake kwa sababu Yezebeli alitafuta kumuua, yawezekana ndani yake alikuwa amekusudia kufika eneo ambalo litakuwa na usalama au eneo ambalo adui hata weza kufika kwa ulahisi.

Lakini alipokuwa kwenye hiyo safari kuna mambo yalimtokea ndani yake, jambo la kwanza alihisi kukata tamaa ya kufika alikokuwa anataka kufika“Akajiombea roho yake afe, akasema, Yatosha, sasa, Ee BWANA, uniondoe roho yangu”,

Jambo la pili; aliishiwa nguvu za kuendelea alikukuwa anaenda.
“Lakini yeye mwenyewe akaendelea katika jangwa mwendo wa siku moja, akaenda akaketi chini ya mretemu”
Yawezekana hata wewe kuna eneo au kituo fulani kwenye maisha yako umekaa kwa mda mrefu sana na umejikuta ukijitamkia maneno ya kuchoka na kukata tamaa ya kuendelea mbele au kuishiwa nguvu.
Kukaa kwenye kituo fulani  au jambo fulani kwa mda mrefu pasipo kuendelea mbele, yaani unatumia nguvu kubwa sana kwenye jambo fulani lakini haufiki unakotaka kufika au unapata matokeo madogo,katika hali hiyo ni wakati mzuri sana ambao marafiki waliokutia moyo wakati unaanzisha jambo fulani kukukimbia na kukudharau.
Ukiona hivyo elewa ya kuwa unahitaji sana ufahamu na nguvu za Mungu kuja ndani yako ili zikusaidie uweze kufika unakotaka kufika, Nguvu hizi na ufahamu huu wa kimungu unapatikana kwa kula chakula cha kiroho.
Eneo hili linahitaji usikivu sana ndani yako na hali ya kufanya au kutekeleza maagizo ya kuinuka na kula chakula, huku ndani yako ukijua ya kuwa bado unasafari ndefu sana kwa hiyo unahitaji kula chakula cha kutosha ili upate nguvu ya kukusaidia kufika unakotaka kufika.
Elewa ya kuwa Mungu tayari kakuandalia chakula cha kukupa nguvu ya kufika unakotaka kufika, chakula hiki unaweza kukipata kupitia mafundisho mbalimbali ya neno la Mungu, lakini tatizo linaweza likawa ndani ya mtu kuwa na upofu wa kiroho au kukosa ufahamu au kwa sababu ya kukata tama tumeshindwa kukiona chakula alichotuandalia Mungu.
Wakati ambapo Eliya alikuwa amechoka na kutamani kufa, ndio ulikuwa wakati ambao Mungu aliachilia chakula kwa Eliya, lakini kama ingetoke Eliya asingekuwa na usikivu wa kuinuk inamaa asingeona chakula lakini angeshindwa kufika alikokuwa anataka kufika.
1 Wafalme 19:6
Akatazama, kumbe! Pana mkate umeokwa juu ya makaa, na gudulia la maji, kichwani pake .Akala akanywa, akajinyosha tena”
Lakini pia upo wakati tunakula chakula katika wakati fulani (neno la Mungu) lakini tumekosa kuwa na ufahamu wa kujua sababu ya kula hicho chakula, matokeo yake tunakula lakini bado tunaendelea kukaa kwenye hicho kituo.
Malaika alimwendea tena Eliya kumsisitiza ale, yawezekana alikula kidogo kwa sababu hakujua ya kuwa alikokuwa anaenda ni mbali, kwa sababu hiyo Malaika alitaka Eliya ale ili asichoke njiani na afike ambapo alitakiwa kufika.
1 Wafalme 19:7
“Malaika wa BWANA akamwendea mara ya pili, akamgusa akasema, inuka, ule; maana safari ni kubwa mno kwako
1 wafalme 19:8
Akainuka, akala, akanywa, akaenda Kwa nguvu za chakula hicho siku arobaini mchana Na usiku hata akifika Horebu, mlima wa Mungu”
Nguvu ya chakula (Neno) inaweza kukusaidia kufika unakotaka kufika, kama tu ukiamua kufutilia na kuchukua maamuzi ya kujifunza neno kwa hali ya juu ili likusaidie katika safari yako ya kufikia jambo fulani kwenye maisha yako lakini pia kuufikia uzima wa milele.
Jambo la msingi sana; Jitahidi sana unapoanza safari ya kufikia jambo lolote lile kwenye maisha yako ,tafuta kwanza kujua uhakika wa nguvu iliyondani yako ya kukuwezesha kufika unakotaka kufika , kama ukikosa uhakika  wa kulifikia hilo jambo ni vyema ukaacha kwenda au kulianzisha hilo jambo. Kaa na Mungu vizuri mpaka upate uhakika wa kutosha juu ya hilo jambo.
Na ikitokea umepata uhakika ndani yako kupitia Roho Mtakatifu, basi hakikisha unafanya au unaendelea mbele ili ulifikie au ufike unakotaka kufika pasipo kuangalia ulipotoka au sauti nyingi za watu, kwa sababu ukingalia nyuma kuna uwezekano wa wewe kujiona kuwa haustahiri kufika huko.
Wapo watu watakao inuka na kukutia moyo unapoanza safari (kimaisha, kiimani, ndoa, mahusiano na mambo mengine), lakini pia wapo wangine wapo kwa ajiri ya kukukatisha tamaa. Maneno ya watu yapo ndugu yangu na kelele nyingi sana za watu, kelele hizi huweza kuongezeka sana.
Acha kusikiliza sana maneno ya watu wanasema nini juu yako kwa ajili ya kukukatisha tamaa ila sikiliza nini Mungu anasema juu yako.

Pata nakala ya kitabu cha somo hili
kwa mawasiliano 0768226595
kapayafarajaph@gmail.com
Mwl Fredrick kapaya
Mungu akubariki sana 

Comments

Popular posts from this blog

HATIMA YAKO

UAMINIFU

NAFSI ILIYOINAMA