UPENDO



USIBEBE CHUKI MOYONI MWAKO ILA BEBA UPENDO


Walawi 19:17

"Usimchukie ndugu yako moyoni  mwako, ni lazima kumkemea jirani yako, wala usichukue dhambi kwa ajili yake usifanye kisasi, wala kinyongo juu ya wana wa watu wako, bali umpende jirani yako kama nafsi yako, mimi ndimi BWANA*"
     

  •  Maana ya neno chuki

Chuki ni hali ya kutompenda mtu au watu au hali ya kuwa na roho mbaya, Chuki pia inaweza kuwa ni hali ya kugombanisha watu, fitina au kukasirika.

Mambo ya msingi kwenye hili somo

Chuki inaweza kutengenezwa na mtu au watu kwa sababu zao wanazozijua wao wenyewe zinaweza kuwa za msingi au zisiwe za msingi.

Moyo huweza kupenda au kuchukia, kwa sababu hiyo upo wakati mtu hupenda na upo wakati mtu huchukia.

Mhubiri 3:8

"Wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia....."

  •  Upo wakati unaweza kuchukia au kuchukizwa na mtu au watu ila hakikisha usiiweke chuki ndani yako.
Wapo watu wanaokuchukia (hawakupendi) ila wewe haujui kama wanakuchukia.

Zaburi 69:4

"Wanaonichukia bure ni wengi kuliko nywele za kichwa changu"

Chuki ni tabia inayoweza kukusababishia wewe usiurithi uzima wa milele

Moyo huweza kubeba upendo juu ya watu au mtu lakini pia moyo unaweza kubeba chuki juu ya mtu au watu. 
  Moyo ukibeba chuki kwa mda mrefu huweza kuharibika, kuchafuka, kupoteza tabia fulani za upendo.
πŸ‘†Utachoka kwa sababu chuki ni mzigo mzito sana moyoni, ukichoka moyo matokeo yake unaweza kufanya maamuzi mabaya yatakayokugharimu wewe na ndugu zako.
  • Chuki inaweza kusababisha mtu awaze mabaya juu ya mtu mwingine.

Mwanzo 27:4

"Esau akamchukia Yakobo kwa ajili ya ule mbaraka babaye aliombarikia. Esau akasema moyoni mwake, siku za kumlilia baba yangu zinakaribia, ndipo nitakapomwua ndugu yangu Yakobo”

Ukibeba upendo hautachoka kwa sababu upendo huleta wepesi ndani ya moyo ila elewa kuwa upendo unagharama. Ukitaka upendo ukae ndani yako au uwapende wengine kubali kuingia gharama
πŸ‘†Mungu aliingia gharama ya kumtoa mwana wake wa pekee ili afe kwa ajiri yetu.

kwanini aliingia gharama?

  •  Kwa sababu alitupenda mno.
Yohana 3:16

"Kwa maana kwa jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanawe wa pekee...."

πŸ‘‰ Mtu akibeba chuki juu ya rafiki yake au ndugu yake basi hawezi au hataweza kusema naye kwa amani.
πŸ‘† Na hata kama akisema naye basi ataongea naye tu kwa sababu imembidi ila kule ndani kutakuwa hakuna amani kabisa wala furaha ya kuendelea kusema naye.

Mwanzo 37:4

"Ndugu zake wakaona ya kuwa baba yao anampenda kuliko ndugu zake wote, wakamchukia, wala hawakuweza kusema naye kwa amani"

  • Usifurahie au kukubari kuendelea kuwa na hiyo hali ya kukosa amani na huyo mtu au watu ila Biblia inasema Kuwa.
Waebrani 12:14

"Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote.... "

1 Yohana 2:9-11

"Yeye asemaye kwamba yupo nuruni, naye amchukia ndugu yake, yumo gizani hata sasa. Yeye apendaye ndugu yake, akaa nuruni ,wala ndani yake hamnakikwazo"

πŸ— Chuki ikibebwa sana moyoni huwa kama ufunguo unaofungua mlango wa kuruhusu giza kuingia moyoni mwako.

πŸ”‘ Upendo ni ufunguo unaofungua mlango kuruhusu Nuru kuingia Ndani ya moyo wa Mtu.

πŸ”ͺ Chuki ni kisu kikali sana ikiingia kanisani au katika kundi la watu, huligawa haraka sana kundi na kutengeneza matabaka makubwa Sana.
Chuki inaweza isiletwe na watu kwenye kundi la watu ila inaweza kuletwa na mtu kwenye kundi la watu.


1 Yohana 4:20

"Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo, kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona"

πŸ‘‰ Haupaswi kabisa kuwa na chuki ndani ya moyo wako au kuwachukia wanaokuchukia ila unawajibu wa kuwapenda wanaokuchukia. 

Endapo utakuwa na chuki halafu unasimama kuhubiri, kuimba, kuomba, basi elewa kuwa kwakweli bado haujamjua vizuri Mungu unayemwabudu.

1 Yohana 4:7

"Wapenzi, na mpendane, kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, ni kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu. Yeye asiyependa hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni pendo”
Usimchukie ndugu yako ila mpende.

1 Yohana 3:15

"Kila amchukiae ndugu yake ni mwuaji : nanyi mnajua ya kuwa kila- mwuaji hana uzima wa milele ukikaa ndani yake"

Mwl Fredrick kapaya


0768226595

Luka 6:27
Mungu akubariki sana

Comments

Popular posts from this blog

HATIMA YAKO

UAMINIFU

NAFSI ILIYOINAMA